STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 23, 2014

Tanzania yapaa FIFA, cheki orodha mpya ya Oktoba

Pambano lililoibeba Tanzania katika orodha mpya ya FIFA
SHIRIKISHO la Kandanda Duniani, FIFA limetangaza viwango vipya vya soka ambapo Tanzania imepanda kwa nafasi tano, huku Ujerumani ikiendelea kung'ang'ania nafasi ya kwanza.
Kwa mujibu wa orodha mpya Tanzania iliyokuwa ya 115 katika orodha ya mwezi Septemba, imepanda hadi nafasi ya 110 hii ni kutokana na ushindi wake wa mabao 4-1 dhidi ya Benin.
Hata hivyo ni kwamba Uganda imeendelea kuwa juu ya nchi zote wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), pamoja na kushuka kwa nafasi tano hadi ya 84.
Algeria ndiyo kinara wa nchi za Afrika ikikamata nafasi ya 15 duniani, wakati Mabingwa wa Dunia Ujerumani imeendelea kushika nafasi ya kwanza duniani ikiziongoza Argentina na Colombia wanaoifuata.
Orodha hiyo inaoonyesha  Ubelgiji, Uholanzi, Brazil, Ufaransa, Uruguay, Ureno na Hispania ndizo zinazofunga 10 Bora, ilihali Ivory Coast waliokuwa wakiiongoza kwa muda mrefu Afrika ikiporomoka hadi nafasi ya 25 Duniani.
Ghana imeshuka kwa nafasi mbili hadi ya 35, wakati Misri imepanda kwa nafasi 23 hadi ya 38 na Cameroon imepanda kwa nafasi mbili hadi ya 40, ikifuatiwa na Senegal na Nigeria ambazo zote zimeporomoka kwa nafasi tano. 
Benin iliyopigwa 4-1 nq Tanzania yenyewe imeporomoka toka nafasi ya 78 hadi 86.
ANGALIA 30 BORA DUNIANI:    1    Germany
    2    Argentina
    3    Colombia
    4    Belgium
    5    Netherlands
    6    Brazil  
    7    France
    8    Uruguay
    9    Portugal  
    10    Spain  
    11    Italy  
    12    Switzerland
    13    Chile  
    14    Croatia
    15    Algeria
    16    Costa Rica
    17    Mexico
    18    Greece
    19    Ukraine
    20    England
    21    Romania
    22    Czech Republic
    23    USA
    24    Slovakia
    25    Côte d'Ivoire
    26    Bosnia and Herzegovina
    27    Ecuador
    28    Iceland
    29    Austria
    30    Russia

No comments:

Post a Comment