STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 24, 2014

Maximo kutumia 4-4-2 na 4-2-3-1 kuiangamiza Stand Utd Shy Town

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/07/118.jpg
Maximo akiwa na msaidizi wake
Na Mwandishi Wetu, Shinyanga
KOCHA wa timu yaYanga, Mbrazil Marcio Maximo amepania kutumia mfumo wa 4-4-2 na 4-2-3-1 ili kupata ushindi dhidi ya wapinzani wao Stand United watakaoumana nao kesho kwenye uwanja wa Kambarage mjini hapa.
Aidha kocha huyo amesema wachezaji wake hawatakuwa na cha kujitetea endapo watashindwa kupata ushindi kwenye mchezo huo ambao umevuta hisia za mashabiki wengi wa soka wa Kanda ya Ziwa.
Maximo alisema, mashabiki wana matumaini makubwa na timu yaio hivyo wana kila sabbau ya kushinda ili kuwaopa moyo mashao hao hasa baada ya  kutoka suluhu dhidi ya mahasimu wao Simba.
"Kiufundi timu ipo vizuri na hakutakuwa na mabadiliko makubwa na kikosi kilichocheza na Simba, kikubwa hatupaswi kuwadharau wapinzani wetu. Nimewambia wachezaji wangu kuwa hatutaeleweka nikipoteza mchezo dhidi ya Stand United," alisema Maximo.
Alidokeza kuwa katika mchezo huo atatumia mfumo wa 4-4-2 na 4-2-3-1 kutokana na uwezo wa wapinzani wao.
"Kasi na uwezo wa wapinzani wetu ndiyo utanifanya niwe nabadilisha mfumokama ilivyokuwa  katika mchezo dhidi ya Simba, najua wapinzani wetu watakuwa kwenye uwanja wao na mbele ya mashabiki wao, ila Yanga ni timu kubwa na tutapambana kupata ushindi," alisema.
"tunataka kumiliki mpira na kutengeneza nafasi ambazo ni lazimawachezaji wazitumie. Nimefanyia kazi mapungufu niliyoyaona kwnye mchezo uliopita ambapo tulikosa umakini katika umaliziaji," aliongeza Mbrazili huyo aliyewahi kuwa kocha wa Taifa Stars.
Kikosi cha Yanga kiliwasili mjini hapa leo Ijumaa kikitokea mjini Dodoma walipokuwa wameweka kambi fupi na kucheza mechi ya kirafiki na CDA mechi iliyoisha kwa timu hizo kushindwa kufungana.
Yanga wanavaana na timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu ikiwa imekusanya jumla ya pointi saba kutokana na mechi nne ikipoteza moja dhidi ya Mtibwa Sugar, kushinda mbili dhidi ya Prisons-Mbeya na JKT Ruvu na kuambulia suluhu kwa watani zao Simba.

No comments:

Post a Comment