STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 24, 2014

Morocco awarejesha Cannavaro, Mwadini, Morris, Znz Heroes

http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2012/12/031.jpg
Cannavaro
http://static.goal.com/157000/157068_heroa.jpg
Morris
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjY-Tu4KKL2CYhZPkBSzjF0-V4kSIPwEJde1qQlonYEs-N85JaNZYuBzwAwmXUlnP3r_o4DAYWaJTu9ryL2LkGOx1M6IxUB1mfmn9MrnmHBS40GN5leNRofQ-ONdsoynTGvokMUgbol-5zE/s1600/IMG_2147.JPG
Dua baada ya kufunga bao
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjrtNXrylghI-on4pxzSCNBKSw2YLL6cuTN4BW1rOKFgkCJSZKgL58-EZTtjgHF0MdcXndeL44bDVqIKMkIAYlQuyq6T8lQzTCbuiT-4_xrtuinOEOIvxIKf0p4gWg8VWKJEZvzHGoN0V-9/s640/SAM_1110.JPG
Kocha Hemed Morocco
KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, Hemed Suleiman 'Morocco' amewarejesha kikosi nyota wa Yanga na Azam, Nadir Haroub 'Cannavaro', Aggrey Morris na mlinda mlango Mwadini Ali.
Akitangaza wachezaji watakafanya mazoezi kwa ajili ya kupata kikosi kitakachoshiriki Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge mwaka huu yatakayofanyika nchini Ethiopia, Morocco, alisema amewaita wachezaji hao  na wengine waliokuwa wametemwa katika michuano ya mwaka jana kwa nia ya kurejesha mshikamano kwa timu yao.
Morocco ameita jumla ya wachezaji 36 ambao watakauwa wanachunjwa mpaka kupata kikosi cha vijana 20 watakaoshiriki michuano hiyo itakayofanyika mwezi ujao.
Kikosi kizima kilichotangazwa na nyota huyo za zamani wa Tanzania na aliyekuwa kocha wa JKt Oljoro na Coastal Union ni pamoja na makipa; Mwadini Ali (Azam), Khalid Mahadhi (Mafunzo), Mudathir Yahya (KMKM) na Mwalimu Ali (Prisons).
Mabeki; Mohammed Othman (Polisi), Said Mussa (Mafunzo), Shafii Hassan (Zimamoto), Ismail Khamis (JKU), Adeyoum Saleh (Chuoni), Edward Peter (Hard Rock), Nadir Haroub 'Cannavaro' (Yanga SC), Nahoda Bakari( Polisi Moro), Aggrey Morris na Abdallah Sebo (Azam), Nassor Masoud ‘Chollo’ na Abdulaziz Makame (Simba SC), Mohammed Faki ( JKT Ruvu) na Khamis Ali (KMKM).
Viungo ni Mohammed Issa (Chuoni), Mohammed Abdulrahim, Ali Juma (Mafunzo), Amour Suleiman (Malindi), Makame Hamad (Zimamoto), Awadh Juma (Simba), Khamis Mcha 'Vialli', Mudathir Yahya (Azam), Abdulhalim Humoud (Sofapaka-Kenya) na Suleiman Kassim 'Selembe' (Polisi Moro).
Washambuliaji; Omar Juma (Hard Rock), Mohammed Seif (Dogomoro), Fasihi Hija (Malindi), Simai Masoud (Fufuni), Nyange Othman, Ibrahim Hilika (Zimamoto), Said Juma ‘Kizota’ (Yanga) na Ame Ali (Mtibwa Sugar).

No comments:

Post a Comment