STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 16, 2014

Everton yaiangamiza QPR, Redknapp maji ya shingo!

QPR striker Bobby Zamora scores against Everton
Bobby Zamora akimtungia Howard
Everton midfielder Ross Barkley
Barkley akifunga bao la kuongoza la Everton kwa shuti kali
KLABU ya Everton usiku wa kuamkia leo wamepata ushindi mwepesi nyumbani baada ya kuifumua QPr mabao 3-1 na kuzidi kukwea katika Ligi Kuu ya England inayozidi kushika kasi.
Ross Barkley alifunga kwa shuti kabla la mita 20 katika dakika ya 33, kabla ya Kevin Mirallas kufungwa kwa mpira wa adhabu ndogo katika dakika ya 43 na mpira wa kichwa wa Steven Naismith kwenye dakika ya 53 yalitosha kuwaangamiza QPR inayonolewa na kocha wa zamani wa Tottenham Hotspur, Harry Redknapp.
QPR ambao kipigo hicho kilikuwa cha nane ugenini katika ligi ya msimu huu, ilipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 80 kupitia Bobby Zamora aliyeuwahi mpira uliotemwa na kipa Tim Howard.
Ushindi huo umeifanya Everton kuitambuka wapinzani wao wa jadi Liverpool wsanaolingana nao pointi 21 na kukaa nafasi ya 10 huku Reds wakiporomoka hadi nafasi ya 11. wakati QPR wamesalia katika nafasi ya tatu toka mkiani wakiwa na pointi 14, nne zaidi ya timu inayoshilikia mkia ya Leicester City.

No comments:

Post a Comment