STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 16, 2014

Jennifer Mgendi 'aifumua' Shelina

Muimbaji na muigizaji filamu, Jennifer Mgendi
MUIMBAJI nyota wa muziki wa Injili nchini ambaye pia ni mtayarishaji na muigizaji wa filamu, Jennifer Mgendi amesema anaifanyia marekebisho filamu yake mpya ya 'Shelina' kuwa filamu fupi ya mfumo wa wimbo ili kuzidi kuwapa raha mashabiki wake.
Akizungumza na MICHARAZO, Jennifer alisema ameona ni vema kuibadilisha 'Shelina' kuwa katika mfumo mwingine ili kuwapa ladha tofauti mashabiki wake ambao wamemzoea katika kazi nyingine alizowahi kuzitoa nyuma.
Jennifer alisema atautumia wimbo wake uitwao 'Kaa Chonjo'.
"Nimeamua kufanyia marekebisho filamu yangu ya 'Shelina' na sasa naitengeneza kama filamu fupi ya mfumo wa wimbo, nikiutumia wimbo wa 'Kaa Chonjo," alisema Jennifer anayejiandaa kuachia albamu yake ya nane iitwayo 'Wema ni Akiba'.
Filamu hiyo ya 'Shelina' inakuja wakati akitamba na kazi yake iitwayo 'Mama Mkwe' ambayo inaendelea kusumbua sokoni.
Mbali na 'Mama Mkwe', Jennifer pia amewahi kutamba na filamu nyingine kama  'Chai ya Moto', 'Joto la Roho', 'Teke la Mama', na 'Pigo la Faraja'.

No comments:

Post a Comment