STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 16, 2014

Manchester Utd yatabiriwa kutwaa ubingwa wa England

http://i.huffpost.com/gen/1226648/thumbs/o-PHIL-NEVILLE-570.jpg?6
Phil Neville enzi akiichezea Manchester United kabla ya kutimkia Everton
USHINDI wa mara sita mfululizo katika mechi zake za Ligi Kuu ya England iliyopata klabu ya Manchester United kumetajwa ni dalili za kurejea kwenye 'fomu' yake na kutabiriwa kutwaa ubingwa wa msimu huu.
Nyota na kocha msaidizi wa zamani wa klabu hiyo, Phil Neville, amenukuliwa akisema kwamba klabu hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa mabingwa wa England baada ya kutulia kutoka kwenye misukosuko ya msimu msimu uliopita.
"Ndiyo wanaweza'' alisema Neville aliyenyakua mataji sita ya Ligi Kuu ya England akiwa kama mchezaji kabla ya kuangukia kuwa miongoni mwa makocha msaidizi chini ya David Moyes aliyetimuliwa.
 "Wachezaji wanaamini wanaweza kutwaa taji na hilo Louis Van Gaal anaweza kulifanya," alisema Neville.
Kauli ya Neville imekuja baada ya Manchester United kupata ushindi wa sita mfululizo kwa kuifumua Liverpool kwa mabao 3-0 katika pambano lililochezwa siku ya Jumapili.
Kabla ya hapo klabu hiyo ilionekana kuyumba kiasi cha mashabiki kuanza kupoteza imani kwa Van Gaal kabla ya kocha huyo kuwatuliza na kuanza kuwapa raha kwa kushinda mfululizo.
Mechi hizo sita za Manchester United iliyoshinda mfululizo ni hizo hapo chini:

8 November:  Crystal Palace 1-0 (nyumbani)
22 November: Arsenal 2-1 (ugenini)
29 November: Hull 3-0 (nyumbani)
2 December: Stoke 2-1 (nyumbani)
8 December: Southampton 2-1 (ugenini)
14 December: Liverpool 3-0 (nyumbani)

No comments:

Post a Comment