STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 16, 2014

Nyota Manchester Utd katika 'kashfa' ya rushwa Hispania

http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Manchester+United+v+Valencia+ODBuEmnisftx.jpg
Ander Herrera anayetuhumiwa kwa upangaji matokeo ya mechi ya La Liga 2011
http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Jefferson+Montero+Exeter+City+v+Swansea+City+Rttkn623zmEl.jpg
Montero naye yumo katika mkumbo huo
http://static.goal.com/187500/187540_heroa.jpg
Nahodha Gabi,  naye anatuhumiwa
http://static.weltsport.net/picmon/e9/dVK_baa3z_l.jpg
Kocha Aguirre

KIUNGO nyota wa Manchester United, Ander Herrera na nahodha wa Atletico Madrid, Gabi ni miongoni mwa wachezaji wanaochunguzwa kwa kujihusisha na tuhuma za upangaji wa matokeo ya mechi ya kufungia msimu wa 2010-2011 wa Ligi Kuu ya Hispania.
Wengine waliohusishwa na kadhia hiyo ni Kocha wa zamani wa Real Zaragoza anayefundisha timu ya taifa ya Japan Javier Aguirre na mchezaji wa Swansea City, Jefferson Montero.
Kwa mujibu wa BBC, Mwendesha Mashtaka wa Idara ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini Hispania Alejandro Luzon, ameiagiza Mahakama kumchunguza kocha wa zamani wa klabu ya Real Zaragoza na baadhi ya wachezaji kutokana na tuhuma za kudaiwa kuuza mchezo dhidi ya Levante.
Katika pambano hilo la kufungia msimu Zaragoza ilishinda mchezo huo kwa mabao 2-1 na kuepuka kushuka daraja, lakini sasa imebainika kuwa matokeo hayo yalipangwa baada ya kutembezwa mlungula.
Upande wa mashitaka uliowasilisha mashtaka yake katika Mahakama mjini Valencia jana Jumatatu, unadai kuwa watuhumiwa wanahusishwa na rushwa ya dola million mbili. 
Baadhi ya wachezaji wanaotuhumiwa katika kashfa hiyo ni Kiungo wa Manchester United aliyewahi kukipiga Zaragoza wakati wa mchezo huo kabla ya kuhamia Athletico Bilbao, Ander Herrera, anayeichezea Manchester United, nahodha wa Atletico Madrid, Gabi, Montero na Javier Aguirre.
Inadaiwa kuwa wachezaji wa Lavante walishikishwa fedha ili kupoteza pambano hilo na kuinusuru Zaragoza isishuke daraja katika pambano la Mei 21, 2011.
Jumla ya watu 41 wakiwamo wachezaji, makocha na wakurugezi wa timu hizo mbili wamehusishwa katika upangwaji huo wa matokeo ya pambano hilo.

No comments:

Post a Comment