STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 16, 2014

Salha wa Hammer avunja ukimya na Kishtobe cha Mtaa

MUIMBAJI nyota wa muziki wa taarab, Salha Abdallah amevunja ukimya baada ya kutoka kwenye likizo ya uzazi kwa kuibuka na wimbo uitwao 'Kishtobe cha Mtaa' uliopo kwenye albamu mpya ya kundi la Five Star Modern.
Akizungumza na MICHARAZO, Salha maarufu kama 'Salha wa Hammer' alisema wimbo huo ni miongoni mwa nyimbo tano zitakazokuwa katika albamu yao itakayozinduliwa Ijumaa wiki hii.
Salha alisema wimbo huo ni wa kwanza kwake tangu alipoenda likizo ya uzazi na kuwataka mashabiki wajitokeze kwa wingi kwenye uzinduzi huo ili kupata uhondo toka kwake na wanamuziki wote wa Five Star.
"Baada ya likizo ya uzazi, hatimaye natarajia kuanza kazi na wimbo wa 'Kishtobe cha Mtaa' ambao nimekiimba mwanzo mwisho nikisaidiana na akina Mwape Kibwana na wengine kitakuwa kwenye albamu itakayozinduliwa Ijumaa," alisema Salha.
Mbali na wimbo huo wa Salha, albamu hiyo ya 'Kichambo Kinakuhusu' ina nyimbo za 'Big Up Dear', 'Ubaya Hauna Soko', 'Sina Gubu Nina Sababu' na 'Kichambo Kinakuhusu' wenyewe.

No comments:

Post a Comment