STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 3, 2015

Arsene Wenger awakata maini wanaotamani aondoke Arsenal

http://www.arsenal.com/assets/_files/scaled/510x250/aug_10/gun__1281108157_20100806_wenger_membersday1.jpg
Kocha Arsene Wenger
KOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amewakata maini wanaodhani fujo wanazomfanyia zinaweza kumfanya aiteme timu hiyo.
Wenger amesisitiza kuwa asingeweza kuondoka katika timu hiyo hata kama wangeshindwa kunyakuwa Kombe la FA msimu uliopita. 
Arsenal walimaliza ukame wao wa vikombe wa miaka tisa kwa kuifunga Hull City kwa mabao 3-2 katika mchezo wa fainali uliofanyika katika Uwanja wa Wembley Mei mwaka jana. 
Akiulizwa na wanahabari kama angeondoka kwa kushindwa kunyakuwa Kombe la FA, Wenger amesema isingewezekana kwani hakuona umuhimu huo. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa katika mechi 1000 alizoisimamia Arsenal ameshinda 600 hiyo inamaanisha ana wastani wa ushindi kwa asilimia 60 hivyo haoni sababu ya kujiuzulu kwani anafanya kazi yake vyema. 
Wenger amesema anaheshimu mkataba wake na ataendelea kuutumikia mpaka hapo wakati wake utakapofika.

No comments:

Post a Comment