STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 3, 2015

Kocha afichua Ronaldo kurudi Manchester Utd

http://img2.timeinc.net/people/i/2012/specials/sma/athletes/cristiano-ronaldo-1-435.jpg
Ronaldo
KOCHA Msaidizi wa zamani wa klabu ya Manchester United, Mike Phelan amesema kuwa nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo anaweza kusikiliza kama klabu hiyo ikijaribu kumnunua tena.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ureno ametengeneza mahusiano mazuri na mashabiki wa klabu hiyo katika kipindi alichoichezea kabla ya kujiunga na Madrid kwa kitita cha paundi milioni 80.
Phelan anaamini kuwa Ronaldo anaweza kurejea United kwani alifurahia katika kipindi chote alichokuwepo hapo kwasababu ndio maisha yake ya soka yalipoanza kung’ara.
Pamoja na hayo Phelan anadhani kwasasa itakuwa mapema mno kwa Ronaldo kurejea Old Trafford hususani kutokana na mafanikio aliyopata na hadhani kama klabu hiyo inaweza kumruhusu.

No comments:

Post a Comment