STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 3, 2015

Equatorial Guinea kumpa ulaji Becker

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/2e/Esteban_Becker_Churukian.jpg/150px-Esteban_Becker_Churukian.jpg
Kocha Becker
WENYEJI wa michuano ya Mataifa ya Afrika, AFCON inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi lake Januari 15, Guinea ya Ikweta wanajiandaa kumpa ulaji kocha Estaban Becker kuchukua mikoba iliyoachwa wazi na Andoni Goikoetxea waliyemtema.
Chama cha soka nchini humo, kiliamua kutomuongeza mkataba kocha huyo Goikoetxea uliomalizika Desemba 31 mwaka jana.
Rais wa chama hicho Andres Jorge Mbomio amedai kuwa wameamua kutomuongeza mkataba kocha huyo baada ya kukiuka masharti ya mkataba wa kwanza kwa kushindwa kusafiri na kikosi cha timu kwenda Ureno Desemba 16.
Guinea Ikweta iliyookoa jahazi la michauno huyo kwa kuipokea Morocco waliogoma kwa dai la tishio la ugonjwa wa Ebola, ina wiki mbili kuandaa kikosi chao kabla ya kuanza kwa michuano hiyo ambapo wao watafungua dimba na Congo Brazzaville Januari 17 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment