STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 3, 2015

David Moyes amuita Steven Gerrard Real Sociedad

https://s.yimg.com/bt/api/res/1.2/fw0doU3LIH0xHkBkFbvYfA--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9ZmlsbDtoPTM3NztpbD1wbGFuZTtweG9mZj01MDtweW9mZj0wO3E9NzU7dz02NzA-/http://media.zenfs.com/en_GB/Sports/Eurosport/1382031-29636997-2560-1440.jpg
David Moyes akipeana mkono na Steven Gerrard
MENEJA wa zamani wa Manchester United, David Moyes amemfungulia milango Steven Gerrard kujiunga na klabu ya Real Sociedad mwishoni mwa msimu huu.
Moyes alikuwa na msimu mbaya wakati akiinoa United msimu wa 2013-2014 hali iliyopelekea kutimuliwa lakini sasa amepewa nafasi nyingine kwa kupewa kibarua cha kuinoa klabu hiyo ya Hispania.
Baada ya Gerrard kutangaza uamuzi wake wa kuondoka Liverpool baada ya mkataba kumalizika, Moyes amempa nafasi ya kufikiria kujiunga na Sociedad ili kupata changamoto mpya.
Moyes mwenye umri wa miaka 51 amesema Gerrard amecheza kwa mafanikio katika klabu yake hiyo na timu ya taifa ya Uingereza hivyo itakuwa ngumu kuziba pengo lake na kama angependa kwenda Hispania kucheza soka anajua kuwa anaweza kumpigia simu.
Naye meneja wa Southampton Ronaldo Koeman pia amedai kuwa katika kikosi chake kutakuwa na nafasi ya Gerrard kama atataka kujiunga nao.

No comments:

Post a Comment