STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 10, 2015

Fainali Mapinduzi ni Simba na Mtibwa

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/simba1.jpg
Simba waliowafuata Mtibwa Fainali za Kombe la Mapinduzi
Mtibwa Sugar (jezi za kijani) watakaoumana na Simba siku ya Jumanne
KLABU ya Simba imefanikiwa kutinga Fainali za michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015 baada ya kuing'oa Polisi ya Zanzibar na sasa wanatarajiwa kukutana na Mtibwa Sugar siku ya Jumanne.
Mtibwa ilifanikiwa kufuzu hatua hiyo mapema leo jioni baada ya kuiondosha kwa mikwaju ya penati 4-3 'wababe' wa Yanga, JKU baada ya kumaliza dakika 90 wakiwa sare ya 0-0.
Simba iliyoonyesha mabadiliko makubwa tangu ianze kunolewa na kocha Goran Kopunovic, walipata nafasi hiyo muda mchache uliopita baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 katika Nusu Fainali ya pili iliyochezwa uwanja wa Amaan. Zanzibar.
Bao lililoipelekea Simba kwenye hatua hiyo na kurejesha kumbukumbu ya nusu fainali ya mwaka 2010 ambapo timu hizo zilikutana na Mtibwa kuibuka wababe kabla ya kwenda kutwaa taji kwa kuilaza Ocean View bao 1-0.
Pia fainali hizo zinarejesha pia fainali ya ABC Top 8 iliyocvhezwa mwaka juzi na Simba kuilaza Mtibwa kwa mabao 4-3.
Mechi hiyo ya faionali itachezwa usiku wa Jumanne kwenye uwanja wa Amaan huku kila timu ikiwa na matumaini makubwa ya kutwaa taji hilo lililokosa mwenyewe baada ya KCCA ya Uganda kutemeshwa hatua ya Robo Fainali baada ya kufungwa kwa penati na Polisi.

No comments:

Post a Comment