STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 10, 2015

JKT Ruvu waikamata Mtibwa Sugar,, yailaza Stand Utd Ndanda

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjjrGUIMxPw7cdxPgyXtAxRJHOSLFdOsz_Yetg7EBn6y-K7pPB3ToQogwImAjfSZceVrbx9aUL72b0URIua7OK30a6XbaCvr5aiWZXfZNKy95h3Kn2aQ1qmkPYpYSe6mpm7NGtNDBnXSwLZ/s640/DSC_0805.JPG
KIkosi cha JKT Ruvu kilichochupa hadi naasi ya pili ikiziengua Yanga na Azam
MAAFANDE wa JKT Ruvu jioni ya leo wamepata ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Stand United ya Shinyanga na kuikamata Mtibwa Sugar ambao wapo kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015.
Samuel Kamuntu na Amos Mgina waliifungia mafaande hao mabao hayo na kuifanya timu hiyo inayonolewa na kocha Fred Felix Minziro katika mchezo uliochezwa uwanja wa Chamazi na kuifanya ifikishe pointi 16 sawa na Mtibwa waliosalia kileleni. Bao la wageni Stand lilifungwa na Mussa Said.
JKT waliotangulia michezo miwili mbele dhidi ya Mtibwa inatoautiana na vinara hao mabao ya kufunga na kufungwa, Mtibwa ikiwa na 11 na kuungwa manne ilihali JKT ikiwa na mabao 10 na kufungwa 9.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mjini Mtwara, wenyeji Ndanda Fc ililazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Polisi Morogoro.
Wageni walitangulia kupata bao kupitia Said Bahanuzi kabla ya wenyeji kuchomoa kupitia Jacob Massawe na kumanya mshambuliaji huyo wa zamani wa Toto African na African Lyon kuikisha bao la tatu msimu huu.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi moja tu itakayowakutanishja wenyeji Mgambo JKT itakayoikaribisha Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.

No comments:

Post a Comment