STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 10, 2015

Real Madrid yazinduka yaipiga Espanol 3-0

Gareth Bale
Bale akishangilia bao lake wakati Real ikiiadhibu Espanyol
Real Madrid v Espanyol
Nacho akishangilia bao lake
LICHA ya kucheza pungufu timu ya Real Madrid imepata ushindi wa mabao 3-0 nyumbani katika  Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Espanyol na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.
Fabio Coentrao alilimwa kadi nyekundu kaytika dakika ya 53, lakini mabao ya James Rodriguez katika dakika ya 12 , Gareth Bale dakika ya 28 na  lile na Nacho la dakika ya 70 yalitosha kuwapa ushindi muhimu Real Madrid iliyoshuhudia nahodha wake, Cristiano Ronaldo akitoka uwanjani bila kufunga bao ikiwa ni mara ya kwanza baada ya muda mrefu msimu huu.
Kwa ushindi hio Madrid wamefikisha pointi 42 na kuiacha Barcelona ikiwa nafasi ya pili na pointi 38 sawa na ilizonazo nazo Atletico Madrid ambazo zinatarajiwa kushuka dimbani kesho.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, Malaga ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 na  Villarreal na hivi sasa Celta Viro ipo dimbani kuumana na Valencia nyumbani kwao na tayari wamekubali bao 1-0.

No comments:

Post a Comment