STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 9, 2015

KICHOMI NI JASHO NA DAMU-BETHA SHAIBU

MSANII na mtayarishaji chipukizi wa filamu nchini, Betha Shaibu amesema 'limemtoka' jasho na damu katika kufanikisha kuitengeneza filamu yake ya kwanza iitwayo 'Kichomi' ambayo inatarajiwa kuachiwa mwezi huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Betha alisema filamu hiyo iliyoshirikisha mastaa kadhaa nchini ni moja ya filamu ya kimapenzi yenye mafunzo makubwa kwa jamii na hasa watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Betha alisema anaomba Mungu filamu hiyo iingie sokoni ili mashabiki waone tofauti iliyopo kati ya kazi hiyo na nyingine kwa namna msuko wa filamu hiyo ulivyo.
"Kwa kweli sijapumua mpaka kazi iingie sokoni, najua mwanzo ni mgumu lakini nimekubali kupambana ili kusimama kwa kutambua nina kipaji kikubwa cha utunzi na uigizaji," alisema Betha.
Ndani ya filamu hiyo ya 'Kichomi', Betha ameshirikiana na wakali kama Hemed Suleiman, Sabrina Omari, Mzee wa Majanga na wengine na imetengenezwa kupitia kampuni ya Red Leaf Entertainment.

No comments:

Post a Comment