STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 9, 2015

Wazee wa 4 waaga Mapinduzi Cup, wapigwa kidude na JKU

* Nusu fainali ni Simba v POlisi, Mtibwa v JKU

BAADA ya kutamba kwa kugawa 'dozi' nono ya mabao manne manne kwa wapinzani wao katika mechi ya makundi kabla ya kupunguzwa na Shaba kwa kuishinda bao 1-0, Yanga imeaga michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kufungwa bao 1-0 na JKU.
Yanga waliosheheni wachezaji 'ghali' na mastaa wanaotamba Afrika Mashariki walishindwa kufurukuta kwa maafande hao wa Jeshi la Kujenga Uchumi visiwani Zanzibar kunakofanyikia michuano hiyo itakayofikia tamati Jumanne.
Bao lililowazima Yanga na kuhitimisha tambo zake liliwekwa kimiani na Amour Omary 'Janja' aliyemfikia Andrey Coutinho aliye na mabao matatu katika orodha ya wafungaji.
Janja alifunga bao hilo lililokuwa la tatu kwake katika dakika ya 72 na kuwaacha vijana wa Hans van der Pluijm wakijilaumu kutokana na kukosa mabao mengi ya wazi katika muda wote wa pambano hilo lililochezwa uwanja wa Amaan.
Ushindi huo kwa JKU imeifanya timu hiyo kutinga Nusu Fainali na kupata nafasi ya kuvaana na Mtibwa Sugar waliowang'oa Azam kwa mikwaju ya penati baada ya kumaliza pambano lao kwa kufungana bao 1-1, Azam wakilazimika kusawazisha dakika za jioni kupitia Kipre Tchetche baada ya Shomar Ally kutangulia kufunga.
JKU imekuwa timu ya tatu kutoka kundi C ambazo zote zimepenya robo fainali na kutinga pia Nusu Fainali.
Nyingine ni Simba ambayo itaumana kesho na Polisi Zanzibar waliowavua taji la michuano hiyo KCCA ya Uganda kwa mikwaju ya penati baada ya kutoka suluhu ndani ya muda wa kawaida na Mtibwa Sugar ambao ni Vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

No comments:

Post a Comment