STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 9, 2015

2014 ni Yaya Toure tena, aweke rekodi akiifikia ile ya Samuel Eto'o

Yaya  Toure aliyenyakua tuzo ya Mwanasoka Bora akiweka rekodi ya aina yake Afrika
Samuel Eto'o aliyekuwa akishikilia rekodi ilivyofikiwa na Toure
KIUNGO wa kimataifa wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya Manchester City, Yaya Toure ameibuka tena kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mara ya nne na kufikia rekodi ya Samuel Eto'o wa Cameroon.
Toure alishinda tuzo hiyo ikiwa ni rekodi ya kuwa mwanasoka wa kwanza kutwaa mara nne mfululizo katika hafila iliyofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Lagos Nigeria.
Toure, 31, aliibuka kidedea kwa kupata pointi nyingi mbele ya mshambuliaji wa Borussia Dortimund raia wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang na kipa wa Nigeria Vincent Enyeama.
Mchezaji huyo aliyeipa City taji la Ligi Kuu msimu uliopita na kuipeleka Tembo ya Ivory Coast kwenye Fainali za Afrika zitakazoanza wiki ijayo, alishatwaa tuzo miaka mitatu iliyopita 2011, 2012 na 2013.

Ni Eto'o pekee aliyekuwa na rekodi ya kutwaa tuzo hiyo mara nne baada ya kufanya hivyo mwaka 2003, 2004, 2005 na 2010.
Katika tuzo nyingine Mwanasoka Bora anayecheza barani Afrika imeenda kwa Firmin Mubele Ndombe (DR Congo), huku Mwanasoka Bora wa Kike tuzo akiwa ni Asisat Oshoala wa Nigeria ambaye pia alinyakua tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike anayechipukia.
Mwanasoka Chipukizi kwa wanaume ilienda kwa Yacine Brahimi (Algeria) wakati tuzo ya Kocha Bora ni; Kheireddine Madoui wa ES Setif.
Timu Bora kwa 2014 ni Algeria kwa wanaume na Nigeria kwa wanawake ilihali Klabu Bora ni ES Setif (Algeria) na Kiongozi Bora ni Rais wa TT Mazembe Moise Katumbi Chapwe.
Orodha ya Mwanasoka Bora Afrika tangu 1995:
1995- George Weah (Liberia)
1996- Nwankwo Kanu(Nigeria)
 1997-    Victor Ikpeba (Nigeria)
1998-    Mustapha Hadji (Morocco)
1999-     Nwankwo Kanu (Nigeria)
2000-    Patrick Mboma (Cameroon)
2001-     El Hadji Diouf (Senegal)
2002-     El Hadji Diouf (Senegal)
2003-     Samuel Eto'o (Cameroon)
2004-    Samuel Eto'o (Cameroon)
2005-     Samuel Eto'o (Cameroon)
2006-    Didier Drogba (Ivory Coast)
2007-     Frederic Kanoute (Mali)
2008-    Emmanuel Adebayor (Togo)
2009- Didier Drogba (Ivory Coast)
2010-     Samuel Eto'o (Cameroon)
2011-     Yaya Toure     (Ivory Coast)
2012-     Yaya Toure (Ivory Coast)
2013-     Yaya Toure (Ivory Coast)
2014-     Yaya Toure (Ivory Coast)

No comments:

Post a Comment