STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 9, 2015

K-One Suma Lee wana ngoma mpya kwa Baucha

BAADA ya kutamba na nyimbo za 'Yule' aliyoimba na Maunda Zorro na 'Jimama Zamiela', msanii K-One anajiandaa kufyatua 'ngoma' mpya aliyomshirikisha mkali wa zamani wa Parklane, Suma Lee.
Akizungumza na MICHARAZO, Mkurugenzi wa Baucha Records inayommilikia msanii K-One, Ali Baucha alisema wimbo huo upo hatua ya mwisho kabla ya kuachia rasmi mwezi ujao ukiwa umetengenezwa katika studio zake.
Baucha alisema wimbo huo ambao bado haujapewa jina ni kati ya kazi tatu mpya za studio hizo zinazotarajiwa kuachiwa karibuni, wimbo mwingine ukiwa ni wa Fizzo aliyemshirikisha Mshindi wa BSS 2013, Walter Chilambo.
"Baucha Records kwa sasa tupo katika maandalizi ya kutoa kazi mpya baada ya kuhamisha studio mahali tulipokuwapo awali pale Magomeni Mapipa, na kati ya kazi hizo moja ni wa K-One akiimba na Suma Lee na mdogo wangu anayeishi Ujerumani pamoja na ule wa Fizzo anaoimba na Walter Chilambo," alisema Baucha mmoja wa watayarishaji mahiri wa muziki wakongwe nchini.

No comments:

Post a Comment