STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 9, 2015

Safari ya Inspekta Haroun Japan sasa April

MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini, Rashid Kahena 'Inspekta Haroun' a.k.a Babu anatarajiwa kwenda nchini Japan baadaye mwaka huu baada ya awali kushindwa kufanya hivyo mwishoni mwa mwaka jana.
Inspekta Haroun aliliambia gazeti hili kuwa, ziara yake kwenda kutengeneza kazi mpya chini ya kampuni ya Hyper Production chini ya Deejay Kay Dee Beatz ilipangwa kufanyika Desemba mwaka jana, lakini ilishindikana baada ya kukosa visa.
Alisema hivyo wamekubaliana na 'mabosi' wake safari hiyo sasa iwe mwezi April akimini kuwa kila kitu kitaenda sawa kwa ajili ya kwenda kufanya kazi chini ya lebo hiyo.
"Safari yangu ya kwenda Japan kuingia mkataba wa kufanya kazi chini ya lebo ya Hyper Production imekwama kwa kukosa visa na sasa itafanyika Aprili kwa kuamini kila kitu kitakuwa kimekamilika, ingawa tayari kampuni hiyo imetengeneza video za nyimbo zangu mbili ambazo nitaziachia hivi karibuni mashabiki wapate burudani," alisema.
Babu alisema video hizo ni za nyimbo za 'Mungu Ndiye Anayepanga alioimba na Sir Juma Nature na ule wa 'Bado Hujachelewa' alioimba pekee yake ambapo kampuni hiyo ilifanya kazi ya kuzichanganya picha na kuongeza vionjo baada ya kuvutiwa na nyimbo hizo.

No comments:

Post a Comment