STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 9, 2015

Sabrina Omar, PHD 'wauza sura' katika KICHOMI

SALOME
PHD
WAIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Sabrina Omar 'Salome' na Hemed Suleiman 'PHD' wanatarajiwa kuonekana kwenye filamu mpya iitwayo 'Kichomi' ambayo imewashirikisha wakali wengine.
Mtayarishaji wa filamu hiyo, Betha Shaibu aliiambia MICHARAZO jana kuwa, filamu hiyo inayotarajiwa kuachiwa sokoni hivi karibuni, ni kazi yake ya kwanza kupitia kampuni ya Red Leaf Entertainment na kuongozwa na Joseph Jembe na Daudi.
Betha alisema filamu hiyo ya kijamii imewashirikisha nyota wakali kadhaa wenye majina nchini akiwamo Salome, Hemed Suleiman 'PHD', Raheem David 'Kibeberu' na Mzee wa Majanga.
"Ni filamu yangu ya kwanza ambayo nimeigiza kwa jina la Jameth nikishirikiana na wakali kama PHD, Sabrina Omar, Kibeberu na Mzee wa Majanga na inatarajiwa kuwa sokoni ndani ya mwezi huu," alisema Betha.
Betha alisema washiriki wa filamu hiyo wameitendea haki na kuwaomba mashabiki wasikose kuiona mara itakatoka hadharani kwani ina mafunzo makubwa kwa jamii mbali na kuburudisha.

No comments:

Post a Comment