STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 13, 2015

TANZANIA YAPOROMOKA FIFA, IVORY COAST YAPAA

https://media.zenfs.com/en_GB/Sports/Eurosport/1411933-30235371-2560-1440.jpg
Mabingwa wa Afrika, Ivory Coast wamepanda kwa nafasi nane
http://api.ning.com/files/Whapl-f-NAa*ff0QY0nKb-GzXt3OU3W0Um6y3Wv2sdGy1YhHgh3eN4BnXYoFkpa8DdbYB3xmtGU1h7gcY39ru0ECvlOuNWgW/TAIFA1.jpg
Tanzania iliyozidi kuporomoka FIFA
 TANZANIA imeporomoka tena kwa nafasi tatu katika viwango vya kila mwezi vya soka vilivyotolewa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) jana.
Tanzania sasa inakamata nafasi ya 30 barani Afrika ikiwa nafasi ya 107 duniani.
Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) unaongozwa na Rwanda ambao ni wa 19 barani Afrika na 72 duniani wakifuatwa na Uganda (21 Afrika, 76 duniani), Ethiopia (28,102), Tanzania, Sudan (32, 112), Kenya (36, 116), Burundi (39, 124), Sudan Kusini (50, 189), Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204 na Djibouti (54, 206).
Algeria wanashika usukani katika 10 bora barani Afrika wakikamata nafasi ya 18 duniani wakifuatwa na Ivory Coast (20), Ghana (25), Tunisia (26), Cape Verde (35), Senegal (36), Nigeria (42), Guinea ya Ikweta (43), Cameroon (45) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (46).
Baada ya kutwaa ubingwa wa Afrika, Ivory Coast imepanda kwa nafasi nane huku wanafainali wenzao, Ghana wakipaa kwa nafasi 12.
Ujerumani wanaendelea kuongoza viwango vya dunia wakifuatwa na Argentina, Colombia, Ubelgiji, Uholanzi, Brazil, Ureno, Ufaransa, Uruguay na Hispania wanaofunga 10 bora ulimwenguni

No comments:

Post a Comment