STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 13, 2015

Aston Villa yamtimua Paul Lambert

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2012/10/4/1349390143504/Paul-Lambert-is-suing-Nor-008.jpg
KLABU ya Aston Villa imetangaza kumtimua kocha wake Paul Lambert baada ya kutofurahishwa na mwenendo mzima wa timu hiyo.
Lambert (45), alirithi mikoba ya Alex McLeish Juni 2012 lakini kutokana na matokeo mabovu, ambayo yameifanya Villa kuburuza mkia katika Ligi Kuu kwa sasa, klabu hiyo ilitangaza kuvunja mkataba na Mscotland huyo juzi.
Taarifa kutoka tovuti ya mtandao huo ilisema: "Aston Villa Football Club jioni hii (juzi) imevunja mkataba na kocha Paul Lambert.
"Kocha wa kikosi cha kwanza, Scott Marshall na  kocha wa makipa Andy Marshall wataendelea kukiandaa kikosi kwa ajili ya mechi ya FA Jumapili dhidi ya Leicester City katika Uwaja wa Villa Park.
Klabu pia ingependa kumshukuru  na kuchukua nafasi hii kumtakia mafanikio mema mbeleni.”

No comments:

Post a Comment