STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 13, 2015

Pigo! Gerrard nje wiki tatu Liverpool

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article4735129.ece/alternates/s1227b/Leicester-City-v-Liverpool.jpg
Nahodha Steven Gerrard
LIVERPOOL, England
NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard anakabiliwa na hatihati ya kuwa nje kwa wiki tatu kutokana na kuwa majeruhi, kwa mujibu wa magazeti mengi ya Uingereza.
Gerrard alitolewa dakika ya 68 wakati Liverpool ikishinda 3-2 dhidi ya Tottenham kwanye Ligi Kuu ya England Jumanne, na magazeti ya The Guardian na Liverpool Echo yameripoti kuwa kiungo huyo anasumbuliwa na misuli ya nyama za paja ambayo yatamfanya kukaa nje kwenye mechi ya Kombe la FA mwishoni mwa wiki dhidi ya Crystal Palace.
Msimu huu Gerrard (34), ameanza mechi 20 za Ligi Kuu na anatarajiwa pia kuikosa mechi ya Europa League nyumbani dhidi Besiktas, nyingine ikiwa dhidi ya Southampton Februari. 22.

No comments:

Post a Comment