STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 8, 2016

Didier Kavumbagu anukia Mbeya City

Didier Kavumbagu (kulia) akiwa na nyota wenzake wa Azam FC
NYOTA wa timu ya Taifa ya Burundi ‘Intamba Mu rugamba’ Didier Kavumbagu anaweza kuwa mchezaji wa kwanza kutangazwa kujiunga na kikosi cha Mbeya City Fc ya jijini Mbeya kinachoshiriki ligi kuu ya soka Tanzania bara muda wowote kuanzia sasa.
Katibu Mkuu wa City, Emmanuel Kimbe, mchana huu ameidokeza mtandao wa mbeyacityfc.com kuwa mazungumzo ya kumnasa nyota huyo wa timu ya taifa ya Burundi aliyekuwa akicheza kwenye kikosi cha Azam Fc ya jijini Dar es Salaam msimu uliomalizika yako kwenye hatua nzuri na tayari wakala wa mchezaji huyo amekwishaainisha yale yote muhimu yanayohitaji kwa ajili ya kuipata huduma yake likiwemo suala la kipengele cha kumruhusu kwenda kufanya majaribio nje ya nchi endapo yatapatikana.
“Tulianza mchakato wa kumpata Kavumbagu mapema kabisa, baada ya kukwama kwenye dirisha dogo Januari mwaka huu, tulikubaliana kuwa hitimisho litakuwa kwenye majira haya ya kiangazi, tayari nimezungumza na wakala wake, tuko kwenye hatua za mwisho kwa sababu ameshaanishia yale yote yanayohitajika, kwa maana hiyo basi, endepo tutamalizia vizuri hatua iliyobaki, muda wowote kuanzia sasa tunaweza kumtangaza kama mchezaji wetu," alisema Kimbe.
Akiendelea zaidi Kimbe alisema kuwa, Kavumbagu ni moja ya nyota walio kwenye orodha ya kocha Kinnah Phiri aliyoomba wasajiliwe ili kuiimarisha timu kwenye eneo la ushambuliaji akilenga kuwa wachezaji wenye uwezo wa kufunga kufuatia tatizo la umaliziaji lililoikuba City  kwenye michezo kadhaa ya mzunguko wa pili wa ligi  licha ya kucheza vizuri kwenye maeneo mengine.
“Tunayo majina  kadhaa ambayo kocha wetu ameomba wasajiliwe kulingana na mahitaji aliyonayo, Kavumbagu anaweza kuwa  wa kwanza kati yao,wengine watafuata kwa mujibu wa taratibu zetu, tunataka kufanya usajili makini ili kuimarisha timu na hatimaye tuwe na kikosi kitakachotupatia matokeo mazuri msimu ujao  hii ni baada ya mapito msimu uliopita”.
Kavumbagu  alianza kuichezea timu ya taifa ya Burundi mwaka 2009 na alikuwa mmoja wa nyota waliokiwakilisha kikosi hicho  kwenye michezo ya kutafuta kufuzu Kombe la Mataifa Afrika 2012 na kufunga mabao 2.
Kwa upande  mwingine   Kimbe  amedokeza kuhusu nyota ambao hawatakuwa sehemu ya kikosi cha City msimu ujao, na kusema kuwa  ni vizuri kuendelea kusubiri  kwa sababu muda si mrefu  taarifa  juu ya hilo itatolewa.

No comments:

Post a Comment