STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 8, 2016

Benteke ambeep Klopp, atasepa kama atamzingua

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article6908832.ece/ALTERNATES/s615b/Liverpool-vs-Bordeaux-Europa-League-Group-Stage.jpg
Benteke
ANAONDOKA. Mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ubelgiji, Christian Benteke amesema anataka kubakia Liverpool, lakini amekiri anaweza kuangalia mahali pengine kama hatakuwepo katika mipango ijayo ya Kocha Jurgen Klopp.
Strika huyo aliyepo na kikosi chao kwenye fainali za Kombe la Ulaya Euro 2016, alijiunga na Liverpool akitokea Aston Villa kwa kitita cha Pauni Milioni 32.5 kiangazi mwaka jana.
Mkataba wake ulikuwa wa miaka mitano lakini amekuwa akishindwa kuonyesha cheche zake Anfield tangu Kocha Klopp alipomrithi Branden Rodgers.
Nyota huyo bado anapenda kuendelea kubakia hapo, lakini kama atakuwa nje ya mipango ya Klopp anaweza kuangalia mahali pengine atakapoweza kupata nafasi ya kucheza.
Akihojiwa Benteke amesema akiwa na umri wa miaka 25 sasa sio kwamba ni mkubwa sana au mdogo lakini muhimu ni kupata muda mwingi wa kucheza.

No comments:

Post a Comment