STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 8, 2016

Man City kumekucha! Yaingia vita ya kumwania Aubameyang

https://i.guim.co.uk/img/media/aa83556e4ff4a53c273d8fc73c14e1e6bd7105d7/0_80_3000_1800/master/3000.jpg?w=620&q=85&auto=format&sharp=10&s=53bd60055f2d7d1fab6d5d30c9526dd8KLABU ya Manchester City inadaiwa ipo mbioni kuingia kwenye orodha ya timu zinazomwania straika wa Borussia Dortmund ma Mchezaji Bora wa Afrika 2015, Pierre-Emerick Aubameyang.
City wana matumaini ya kumsana nyota huyo wa kimataifa wa Gabon mwenye umri wa miaka 26 katika kipindi hiki cha kiangazi. Aubameyang anatajwa kuwa mmoja kati ya washambuliaji bora Ulaya baada ya kuonyesha kiwango kikubwa Dortmund akifunga mabao 39 katika mashindano yote msimu uliopita.
Meneja mpya wa klabu hiyo, Pep Guardiola anafahamu vyema kipaji cha Aubameyang na ameona kuwa anaweza kumfaa katika mipango yake ya baadae. City wanadaiwa kuwa tayari kumsaidia Guardiola katika usajili kwa kujiandaa kuvunja rekodi ya usajili kwa kumleta nyota huyo Etihad.

No comments:

Post a Comment