STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 8, 2016

Rais Obama ayakosa mazishi ya Muhammad Ali

http://cdn-mf1.heartyhosting.com/sites/mensfitness.com/files/styles/photo_gallery_full/public/ali_rotator.jpg?itok=CnLNStFo
Muhammad Ali enzi za uhai wake
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/06/382dab0f0ef23504d829de029e0e543f-702x336.jpgMWILI wa bingwa mara wa tatu wa Dunia kwa uzito wa juu, Muhammad Ali unatarajiwa kuzikwa keshokutwa Ijumaa, lakini cha kusikitisha ni kwamba hatazikwa na Rais wa Marekani, Barack Obama.
Muingiliano wa mazishi hao wa shujaa huyo na mwanaharakati wa kuwatetea watu weusi kupitia ngumi, kiasi kwamba leo Marekani inaongozwa na Rais mwenye asili ya Afrika na yale ya mahafali za binti wa Obama ndio sababu ya Obama kukosa mazishi hao.
Viongozi kadhaa kutoka sehemu mbalimbali duniani watakuwa miongoni mwa maelfu ya waombolezaji watakaohudhuria mazishi hayo huko Louisville, Kentucky ambako Ali alizaliwa mwaka 1942.
Ikulu ya Marekani imesema kuwa Obama na mkewe Michelle wanatarajiwa kuwa katika mahafali ya binti yao Malia huko Washington, DC.
Ali alifariki dunia wiki iliyopita hospitalini huko Phoenix, Arizona akiwa na umri wa miaka 74.
Hata hivyo familia ya Obama inatarajia kutuma barua kwa familia ya Ali ambayo itawasilishwa na mshauri mwandamizi wa Ikulu Valerie Jarrett ambaye anamfahamu Ali.
Msemaji wa familia ya Ali, Bob Gunnell amesema Obama alizungumza na mjane wa Ali, Lonnie katika simu kumpa pole kwa kifo hicho cha mumewe. Miongoni mwa viongozi watakaohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Mfalme Abdullah wa Jordan.

No comments:

Post a Comment