STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 8, 2016

Malinzi amlilia Stephen Keshi aliyefariki leo

http://stargist.com/wp-content/uploads/2014/05/Stephen-Keshi-Stargist.jpg
Keshi enzi za uhai wake
NAHODHA na Kocha wa zamani wa Nigeria, Stephen Keshi amefariki dunia ghafla leo Jumatano na kuleta mshtuko mkubwa kwa mashabiki wa soka nchini humo na kwingineko Afrika.
Nchini Tanzania  Rais wa Shirikisho la Soka(TFF), Jamal Malinzi naye ni miongoni mwa walioshtushwa na kifo hicho na kuweka bayana alivyopokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo0 wa Keshi (54) na kutuma salamu zake za pole. Rais Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Nigeria (NFF), Amaju Pinnick, familia ya marehemu Keshi pamoja na ndugu, jamaa, marafiki walioguswa na msiba huo wa gwiji huyo aliyepata kuwa nahodha wa kikosi cha Taifa Nigeria ‘Super Eagles’.
Katika rambirambi ambazo zimefika pia katika Ofisi za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Rais Malinzi amesema kuwa japo Keshi ametangulia mbele za haki, mchango wake kwenye soka hautasahaulika kwani atabaki kuwa alama ya maendeleo ya mchezo wa soka.

No comments:

Post a Comment