STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 8, 2016

Jose Mourinho aanza mambo Man United

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/article_large/public/thumbnails/image/2016/06/08/13/eric-bailly-2.jpg
Eric Bailly
MBONA mtamkoma. Kocha Mkuu wa Manchester United, Jose Mourinho ameanza makeke yake baada ya klabu yake kumnasa beki wa Villarreal, Eric Bailly.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 22 amejiunga na United kwa ada ya Pauni Milioni 30 na kupewa mkataba wa miaka minne.
Akihojiwa Bailly amesema ndoto zake zimetimia za kujiunga na United na kucheza soka katika kiwango cha juu kama siku zote alivyotaka iwe.
Kocha Mourinho amesema Bailly ana nafasi kubwa ya kuja kuwa mmoja wa wachezaji bora duniani.
Bailly alijiunga na Villarreal kwa kitita cha Pauni Milioni 4.4 Januari mwaka 2015 na kucheza katika kila mechi wakati Ivory Coast ikishinda taji la Mataifa ya Afrika wiki chache baadae.
Huo unakuwa usajili wa kwanza wa Mourinho toka atue Old Trafford huku pia wakitajwa kumwania pia mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic.

No comments:

Post a Comment