STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 22, 2016

Real Madrid yathibitisha kumrudisha Morata Santiago Bernabeu

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/09/15/21/2C5ADD7700000578-3235796-image-a-30_1442348975933.jpgWAMEPANIA si mchezo. Mabingwa wa soka Ulaya, Real Madrid wamethibitisha kuwa Alvaro Morata atarejea Santiago Bernabeu kipindi hiki cha kiangazi. Taarifa z klabu hiyo zinasema kuwa, hakuna kizuia kwa mkali huyo kurudia nyumbani.
Awali taarifa za mapema kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Juventus Beppe Marotta zilibainisha kuwa Morata anategemewa kurejea Madrid.
Madrid walikuwa na nafasi ya upendeleo ya kumnunua tena Morata mwenye umri wa miaka 23, ikiwa ni sehemu ya mkataba uliopelekea nyota huyo wa kimataifa wa Hispania kujiunga na Juventus miaka miwili iliyopita na sasa wamethibitisha kufanya hivyo.
Katika taarifa yao iliyotumwa katika mtandao, klabu ya Madrid walithibitisha taarifa hiyo na kudai kuwa Morata atajiunga na mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya wa La Liga chini ya Kocha Zinedine Zidane.
Hata hivyo, taarifa hizo zinadai kuwa Madrid wanaweza kumuuza Morata kwa klabu nyingine ili wapate faida zaidi.

No comments:

Post a Comment