STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 22, 2016

Zaidi ya watu 30 wauwawa Libya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhCVr1da4GQufI6f7fv74iiVc0627Y6UABJL2guBHijQ6toVF7TK8gi380ZbSoUtUUVH7wRW8kPQLhJ84quuCFQ70x6TfQm4AOJ0kHsrTISXMtUavqoZf2nwsmqE0FxYfqDzLHlJRby3gE/s1600/Wapiganaji+wa+NTC+mjini+Sirte.jpg
Picha haihusiani na taarifa hii
SIMANZI. Zaidi ya watu 30 wamepotea maisha katika mapigano baina ya Jeshi la Libya na wapiganaji wa kikundi cha IS.
Inaelezwa mapigano hato yamesananisha vifo hivyo, huku mamia wakiachwa majeruhi, kipindi hiki ambacho waumini wa Kiislam wapo kwenye Mfungo wa Ramadhani.
Kwa mujibu wa BBC Swahili, Msemaji wa hospitali moja alisema kuwa wapiganaji 36 wameuawa huku wengine karibu 140 wakijeruhiwa katika mji wa Sirte ambao ni ngome ya Islamic state.
Wakati huo huo taarifa zinasema kuwa idadi ya watu waliouawa wakati mlipuko ulitokea katika ghala la silaha kwenye mji ulio magharibi wa Garabulli imeongezeka hadi watu 29.
Ghala hilo liliripotiwa kuwa ndani ya kambi inayotumiwa na wapiganaji kwenye mji wa Misrata pwani ya nchi.

No comments:

Post a Comment