STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 21, 2012

Licha ya bahati, lakini tulistahili taji-Cole

BEKI wa Chelsea, Ashley Cole amesisitiza kwamba uwezo wao, sio bahati, ndio kilichowapa ubingwa wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika fainali usiku wa kuamkia jana. Cole, ambaye alifunga moja ya penalti za wakati wa kupigiana "matuta", alikiri kwamba Chelsea ilikuwa na bahati ilikuwa kwao katika fainali wakati Bayern Munich wakipotena zafasi nyingi nzuri za kushinda lakini mwisho wa mechi wao walikuwa washindi waliostahili. Aliiambia Sky Sports 1: "Maneno yamenikauka. Tulipaswa kuwa tumeshafungwa kutokana na nafasi nyingi walizitengeneza. "Tulikuwa na bahati, unahitaji bahati katika michuano hii kama unataka kuwa bingwa. Leo tulikuwa na bahati lakini pia tulistahili kushinda leo." Alipoulizwa hadhani kwamba bahati yao ilikuwa inaelekea kupotea baada ya Bayern kupata penalti dakika tano katika muda wa dakika 30 za nyongeza, mchezaji huyo wa kimataifa wa England aliongeza: "Hapana, kutokana na wachezaji tulionao tulifikiria, 'ok ni penalti lakini bado muda upo', na pale Petr alipookoa kiufundi yale ndiyo yunayoamini daima." Ubingwa ulimaanisha kwamba mara hii bahati ilikuwa upande wa Cole katika fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa baada ya kupoteza mechi za fainali wakati akiichezea Arsenal mwaka 2006 na Chelsea 2008. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye wakati akihamia katika klabu hiyo inayomilikiwa na tajiri alituhumiwa kuwa alifuata pesa na akapachikwa jina la "Cash-ley" Cole alisema: "Hii ndiyo sababu niko hapa." (Mail)

No comments:

Post a Comment