STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 22, 2012

Viuno vya Shilole hadharani

NYOTA wa filamu aliyetumbukia kwenye fani ya muziki, Zuwena Mohammed 'Shilole' amefyatua wimbo mpya uitwao 'Viuno kwa Viuno' ameanza kuusambaza jana Jumatatu. Kisura huyo, alisema kibao hicho ambacho ni cha tatu kwake baada ya awali kuachia 'Lawama' na 'Dume Dada' vinavyokimbiza nchini kwasasa, ameshirikiana kuimba na wakali Kalidjo Kitokololo wa Fm Academia na Rich Mavoko. Shilole, alisema amepanga kuusambaza katika vituo mbalimbali vya redio leo ili uanze kuchezwa hewani, huku akijipanga kuachia nyimbo nyingine kwa ajili ya kuhitimisha albamu aliyopanga iwe na nyimbo sita au nane. "Nimekamilisha kibao kipya kiitwacho 'Viuno kwa Viuno ambao nadhani nitaanza kuusambaza redioni siku ya Jumatatu (jana ili uanze kurushwa hewani," alisema. Shilole, alisema anaamini kama ilivyokuwa kwa nyimbo zake mbili za awali, hata 'singo' hiyo itawabamba mashabiki kutokana na namna ulivyoandaliwa na kazi kubwa iliyofanywa nae na wasanii alioshirikiana nao. "Nataka kuwathibitishia mashabiki wangu, sijavamia fani, bali nauweza muziki kwa vile ni kipaji cha kuzaliwa licha ya kwamba naonekana ni mkali zaidi katika filamu," alisema. Mwanadada huyo, ambaye hujishughulisha na ujasiriamali, alisema mbali na kujipanga kutoa albamu pia anaendelea na maandalizi ya kupakua filamu zake binafsi.

No comments:

Post a Comment