STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 22, 2012

Kumekucha Miss Kurasini 2012

WAREMBO 16 wanatarajiwa kupanda katika jukwaa la ukumbi wa Equator Grill jijini Dar es Salaam Ijumaa ya May 25 katika shindano la kumsaka Miss Kurasini 2012. Mkurugenzi wa ZUM Fashion & entertainment,inayoandaa shindano hilo Zuwena Mustapha alisema jana kwamba maandalizi kwa ajili ya shindano hilo yanaendelea vema na kwamba mwaka huu wataendeleza historia ya kutoa mrembo bomba atakayetikisa hadi ngazi ya Taifa. Alisema mpaka sasa wameshapatikana wadhamini 14 kwa ajili ya kusaidia shindano hilo ambalo linatarajiwa kuwa bomba, huku likiambatana na burudani kabambe.Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Top Model wa Miss Tanzania 2011, Mwajabu Juma (pichani). “Leo napenda kuwaambia kuwa hadi sasa tunajumla ya wadhamini 14 ambao wamejitokeza kudhamini shindano hilo, lakini bado milango ipo wazi kwa yeyote anaependa kutuzamini na kusaidia warembo wetu wa kurasini kupata zawadi nono na shindano kuwea zuri,”alisema Mustapha. Mustapha alisema wadhamini wakuu wa shindano hilo ni Nameems Wear wakisaidiwa na kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redds, Dodoma wine, Clouds FM, Lady Pepeta, Father Kidevu Blog, Jambo Leo, Aucland Tours & Safaris, Candy Bureau de Change, Flexip, PJ Amusement, Renzo Salon na Madishisha Video Production. Aliwataja warembo waliopo kambini na kunolewa na Mwajabu Juma akisaidiwa na Malkia wa vipaji wa Miss Tanzania 2011, Rose Hurbert ni Mariam Sadic (19), Johari Juma (20),Linda Deus (20),Irene Sostheness 20),Neemadoree Sylvery(29),Edna Magige (22), Lindanancy Joseph(20), Elizabeth Mkende (19), Betty Peter (22), Jennifer Njabili (18), Lilian Joseph (20), Farida Mrope (23),Christina Moses (20), Angle Gasper (19), Flaviana Maeda(22) na Sia Kimambo (19).

No comments:

Post a Comment