STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 22, 2012

Mr Nice akamailisha albamu, atamba itamtoa

MSANII anayefurukuta kurejesha makali yake ya zamani, Lucas Mkenda 'Mr Nice' amekamilisha albamu yake mpya itakayofahamika kwa jina la 'Tabia Gani'. Albamu hiyo inatarajiwa kuingizwa sokoni muda wowote kuanzia sasa, itakuwa na nyimbo nane zilizoandaliwa chini ya mtayarishaji nyota, Lamar wa Fishcrab Records. Akizungumza na MICHARAZO, Mr Nice alisema albamu hiyo imekamilika na sasa wanafanya mipango ya kuiigiza sokoni baada ya kutambulishwa na vibao viwili vya 'Tabia Gani' na 'Nionje' alioimba na Muimbaji Bora wa Kiume nchini, Barnaba. Mr Nice alizitaja nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo kuwa ni 'Tabia Gani' yenyewe, 'Nionje', 'Kupata', 'Maneno Maneno', 'Mfalme', 'Nionaje', 'Amini' na 'Ulisemaje'. "Kaka nimekamilisha ile albamu yangu mpya ya kunirejesha upya katika ulimwengu wa muziki baada ya kimya cha muda mrefu, itakuwa na nyimbo nane na kwa sasa najipanga na wasimamizi wangu ili kuiingiza sokoni," alisema. Mr Nice, alisema kwa namna albamu hiyo ilivyoandaliwa na Lamar, huenda akarejesha heshima na makali yake yaliyomfanya abatizwe jina la 'Mfalme wa TAKEU'. "Ni moja ya kazi yenye kiwango cha hali ya juu, si unajua makali ya Lamar na ukichanganya na vionjo vyangu vya 'TAKEU Reloaded', sina shaka itabamba sokoni," alisema. Mr Nice, aliyevuma miaka saba iliyopita na nyimbo matata kama 'Fagilia', 'Kikulacho', 'Friday Night', 'Bwana Shamba' na nyingine, ameibuka upya baada ya kushindwa kusimama hata alipojitosa kwenye muziki wa Injili alipotoa albamu ya 'Fungu la Kukosa'.

No comments:

Post a Comment