STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 22, 2012

Warembo Redd's Miss Bagamoyo waanza kambi Dar

WAREMBO 10 waliojitokeza kushiriki kinyang'anyiro cha kumsaka kisura wa Bagamoyo 'Redd's Miss Bagamoyo 2012', wameanza rasmi kambi ya mazoezi jijini Dar. Mkurugenzi wa Asilia Decoration inayoratibu shindano hilo, Awetu Salim, alisema warembo hao wameanza kambi katika ukumbi wa Meridian Hotel, iliyopo Kinondoni tayari kujiwinda na mchuano huo utakaofanyika Juni 15, mjini Bagamoyo, Pwani. Awetu, alisema kambi hilo ilianza Jumapili na itaendelea hadi siku ya shindano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Sanaa, TaSUBA- Bagamoyo. Mratibu huyo aliwataja baadhi ya warembo hao watakaokuwa chini ya mkufunzi wao Sadah Salim kuwa ni Julieth Jeremiah, Rose Lucas, Beatrice, Rachel, Celine Wangusu na Maria. Aliongeza, kwa kushukuru kujitokeza zaidi kwa wadhamini akiitaja kampuni ya Kishen Enterprises ilijitokeza hivi karibuni kuwapiga tafu katika shindano lao. Awetu, alisema wadhamini hao wapya wameungana na wale wa awali ambao baadhi ni Twanga Pepeta', Kiu Investment, Asilia Boutique & Hair Dressing, Dr Osborn na Dk Kalenga. Juu ya burudani itakaowasindikiza warembo hao, mratibu huyo aliitaja bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' ndio watakaotumbuiza ukumbini siku ya onyesho lao.

No comments:

Post a Comment