STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 27, 2012

Kipa wa zamani Yanga kwenda Msumbiji


KIPA wa zamani wa timu za Yanga na Moro United, Steven Marashi, anatarajiwa kuondoka nchini mwishoni mwa wiki kwenda nchini Msumbiji kujaribu kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Ligi Kuu nchini humo.
Akizungumza na MICHARAZO, Marashi, aliyeachwa kitatanishi misimu miwili iliyopita pamoja na akina Wisdom Ndhlovu na John Njoroge, alisema mipango ya safari yake inafanya mmoja wa mawakala waliopo nchini Msumbiji aliyewahi kumuona akicheza.
Marashi, alisema japo jina la timu anayoenda kufanyiwa majaribio haikumbuki kwa jina, lakini amedai ni ya Ligi Kuu ya Msumbiji na imani yake ni kufanya vema.
"Kaka nipo katika maandalizi ya safari ya kwenda Msumbiji kwa ajili ya kujaribu kucheza soka la kulipwa baada ya kupatiwa na nafasi na mmoja wa mawakala wa nchini humo aliyevutiwa nami wakati nikiwa Moro United," alisema.
Kipa huyo ambaye aliamua kujiengua Moro United mara baada ya kushuka daraja toka Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita, alisema kama mambo yataenda yalivyopangwa basi ataondoka nchini Jumamosi au Jumapili.

No comments:

Post a Comment