STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 27, 2012

Tutegemee vipaji sio miili yetu-Salha

Salha Abdallah katika pozi


MUIMBAJI wa kundi la taarab la Dar Modern 'Wana wa Jiji', Salha Abdallah, amewataka wasanii wenzake wa kike kujiheshimu, kujiamini na kutumia vipaji vyao kuwakomboa kiuchumi badala ya kuitegemea miili yao kujitajirisha.
Salha anayetamba kwa sasa na kibao alichokitunga na kukiimba cha 'Nauvua Ushoga', alisema msanii anayetegemea kipaji chake, kujiheshimu na kujiamini hawezi kukubali kukudhalilishwa na watu wachache wanaowaozunguka katika fani na ndani ya jamii.
Alisema wasiojiamini na siyo na vipaji vya kweli ndio wamekuwa wepesi kujidhalilisha kwa kuitegemea miili yao kuwapa mafanikio na mwishowe kuachwa wakiwa hawana thamani mbele ya watu waliowachezea na jamii kwa ujumla.
"Lazima niseme ukweli wapo baadhi ya wasanii wenzetu wanaitegemea miili yao kuwainua kisanii na kimaisha, ila hawatambui waavyojishushia hadhi, mwanamke wa kweli ni yule anayejiamini, kujiheshimu na kutegemea kipawa alichojaliwa," alisema.
Alisema kama msanii mrembo amekuwa akikutana na vishawishi vingi toka kwa wanaume wakware, ila amekuwa akiwakwepa kistaarabu huku akifichua wengi wa wanaume wa hivyo huandika namba zao za simu katika fedha wanaozoenda kuwatunza.
Muimbaji, aliyezaliwa pacha na mwenzake, alisema binafsi huwa anakerwa na wasanii wa kike wanaojihusisha na skendo na kukubali kutolewa picha za ovyo magazetini.

No comments:

Post a Comment