STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 27, 2012

Wasanii, Airtel wamlilia Sharo Milionea

Meneja Uhusiano wa kampuni ya Airtel, Jackson Mbando

Sharo Milionea enzi za uhai wake
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imeungana na watanzania wengine kumlilia msanii nyota wa filamu na mwanamuziki wa kizazi kipya, Husseni Ramadhani Mkiety 'Sharo Milionea' aliyefariki usiku wa kuamkia jana kwa ajali ya gari.
Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando, alisema wameshtushwa na kusikitishwa na kifo cha ghafla cha Sharo Milionea ambaye waliingia naye mkataba hivi karibuni ili kutangaza huduma za kampuni hiyo.
Alizungumza asubuhi hii na kituo cha Cloud FM, Mbando alisema kifo cha Sharo Milionea, kimewatia simanzi kutokana na ukweli kimekuja ghafla mno na huku akiwa bado anahitajika katika kuitangaza kampuni yao.
"Tunaungana na familia, ndugu na jamaa na wadau wote wa burudani kutokana na kifo cha Sharo Milionea, alikuwa kijana mdogo, mchangamfu na aliyekitumia vema kipaji chake cha sanaa, Airtel tumeguswa na msiba huu kwani tulikuwa bado tunamtegemea kutangaza huduma zetu," alisema Mbando.
Wasanii wengine waliowahi kufanya kazi na msanii huiyo aliyefariki jana saa mbili usiku baada ya gari alilokuwa akiliendesha kwenda kwao Muheza Tanga, kupinduka na kusababisha kifo chake wamedai wanashindwa kuamini kama amefariki.
Masai Nyota Mbofu, amedai itamchukua muda mrefu kumsahau Sharo aliyewahi kutamba naye keenye filamu na kipindi cha 'Vituko Show' wakati kampuni ya Al Riyamy.
Naye mtayarishaji wa filamu nchini Mustafa Wazir 'West' alisema atamkumbuka daima Sharo Milionea kwa kipaji alichokuwa nacho.
Mchekeshaji mwingine aliyekuwa akiigiza na Sharo, Ally Boffu 'Man Bizo', alidai mpaka sasa haamini kama Sharo Milionea amemtoka kwa jinsi ilivyokuwa ghafla.
Kifo cha Sharo Milione kimekuja huku wadau wa sanaa wakiendelea kuwaomboleza muimbaji wa TOT-Taarab Mariam Khamis 'Paka Mapepe' aliyefariki wiki mbili zilizopita na waigizaji Mlopero na John Maganga waliokufa wiki iliyopita.
Hussein Mkiety 'Sharo Milionea, aliyezaliwa Machi 20, 1987 Muheza, akiwa mtoto wa mwisho kati ya watoto watatu na amefariki akiwa mbioni kufyatua video za nyimbo zake mbili zilizokamilika hivi karibuni za 'Vululuvululu' alioimba na Tundaman na 'Changanya Changanya' alioimba na Ally Kiba.
Taarifa tulizozipata hivi tunde zinasema kwamba huenda marehemu Sharo Milionea akazikwa leo mjini Muheza, Tanga ingawa tunaendelea kufuatilia taarifa zaidi juu ya msiba huo.

No comments:

Post a Comment