STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 27, 2012

Wolper amkumbuka marehemu Kanumba

Jacklyne Wolper alipoigiza na Kanumba katika filamu ya Ndoa Yangu


NYOTA wa filamu nchini, Jacklyne Wolper, amemkumbuka marehemu Steven Kanumba na kumtungia filamu iitwayo 'After Death' aliyowashirikisha baadhi ya wasanii chipukizi walioibuliwa na Kanumba enzi za uhai wake.
Muongozaji wa filamu hiyo, Leah Richard, aliiambia MICHARAZO kuwa  filamu hiyo ni maalum kwa ajili ya kuenzi mchango wa mkali huyo wa filamu aliyefariki ghafla na kuzikwa Aprili mwaka huu.
Leah alisema filamu hiyo imetungwa na Jacklyne Wolper aliyewahi kucheza na Kanumba filamu mbalimbali ikiwemo 'Ndoa Yangu' na imeongozwa na yeye.
"Imetungwa na Wolper na kuongozwa na mimi mwenyewe na mpaka sasa imekamilika na inasubiriwa kufanyiwa uzinduzi rasmi hapo baadae," alisema Leah.
Mwanadada huyo alisema anaamini filamu hiyo itakapoingia sokoni itawarejeshea kumbukumbu wapenzi wa filamu juu ya Kanumba na watoto wake kwa namna mtu aliyeigiza kama Kanumba kushabihiana naye kwa sura kwa kiasi kikubwa.
"Yaani ni kama Kanumba amerejea upya ulimwengu kupitia 'After Death' kwa namna aliyemuigiza kufanana naye na namna alivyoigiza na watoto hao wa Kanumba," alisema.
Kanumba, aliyekuwa akifahamika kama The Great', aliwaibua watoto wenye vipaji  na kuigiza nao katika filamu kadhaa kama 'Uncle JJ', 'This is It' na 'Big Daddy', alifariki dunia Aprili 6 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment