STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 27, 2012

Ruvu Shooting wamsubiri Mkwasa



UONGOZI wa klabu ya soka ya Ruvu Shooting ya Pwani, umesema wiki hii utaweka hadharani mikakati yao kwa ajili ya maandalizi ya duru lijalo la Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kupokea taarifa na mapendekezo ya kocha wao.
Afisa Habari wa Ruvu, Masau Bwire aliiambia MICHARAZO kwamba panga pangua ya kikosi chao inatarajiwa kufahamika wiki hii baada ya kumaliza kucheza mechi zao za duru la kwanza kwa kuilaza Prisons-Mbeya mabao 2-0.
Bwire, alisema uongozi unasubiri ripoti ya bnchi lao la ufundi chini ya kocha Charles Boniface Mkwasa, ili kujua wapi pa kuanzia katika maandalizi ya duru hilo walilodai wamelipania ili wamalize msimu katika nafasi nzuri.
"Baada ya kumalizika kwa pambano letu na Prisons tukishukuru kushinda kwa mabao 2-0, kwa sasa tunasubiri taarifa na mapendekezo ya mwalimu wetu kwa ajili ya kujipanga kwa duru lijalo," alisema Bwire.
Bwire, alisema wangependa kuona duru lijalo wakifanya vizuri zaidi na duru lao la kwanza lililowaacha wakiwa nafasi ya saba wakijikusanyia jumla ya pointi 20 kutokana na mechi 13 ilizocheza katika duru hilo.
Afisa Habari huyo, alisema yapo baadhi ya mapungufu yaliyoonekana katika kikosi chao yanayohitajika kurekebishwa, lakini uongozi hauwezi kusema lolote mpaka waipate ripoti ya kocha Charles Boniface.
***

No comments:

Post a Comment