STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 12, 2013

Baby Madaha kutega videoni kidigitali

Baby Madaha katika pozi

LICHA ya kulia na mfumo wa digitali akidai unawalaza kwa kazi zao kutotangazika kama zamani, msanii mahiri wa muziki na filamu nchini, Baby Madaha, ameachia video ya wimbo mpya uitwao 'Nitege'.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema video hiyo iliyotengenezwa na watalaam Tudd Thomas na Nash Disigner, siku yoyote anatarajia kuisambaza ili irushwe hewani na vituo vya runinga.
Alisema ameona haja jinsi zaidi ya kutoa video hiyo, kutokana na ukweli ilikuwa imeshakamilika wakati Tanzania ikiingia kwenye digitali.
"Katika muziki nimetoa video ya Nitege, lakini shaka na namna itakavyotangazika ukilinganisha na kazi zangu za nyuma kutokana na mfumo mpya wa urushwaji wa matangazo ya kidigitali,"alisema Madaha.
Alisema mashabiki wao wameshindwa kumudu kununua ving'amuzi, hivyo anakuwa na mashaka na kazi yake itatangazika vipi, ingawa ameamua kukomaa hivyo hivyo.

No comments:

Post a Comment