STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 12, 2013

KIVUMBI LIGI YA MABINGWA ULAYA KUANZA KUTIMKA LEO

Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake ambapo kesho atakivaa kikosi chake za zamani Manchester United

KIVUMBI cha hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kinaanza leo kwa kushuhudiwa timu nne kuanza kusaka tiketi ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo.
Celtic ya Uskochi itakuwa uwanja wa nyumbani kuwakaribisha mabingwa wa Italia, Juventus, huku Valencia watamenyana na vinawa wa Ligi ya Ufaransa Paris Saint Germani.
Mechi zote hizo zitachezwa kuanza saa 4;45 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, kabla ya kesho mashabiki wa soka ulimwengu kuishuhudia dunia 'ikisimama' kwa muda kupisha pambano la Real Madrid ya Hispania dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester United.
Pambano hilo linasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa timu zote kutokana na uwepo wa Criastian Ronaldo aliyewahi kuichezea na kuipa mafanikio Manchester United ambapo leo atakuwa akiiongoza Real kusaka ushindi kabla ya mechi ya marudiano mwezi ujao.
Pambano jingine la leo litazikutanisha timu za Shakhtar Domestic dhidi ya Borrusia Dortmund ya Ujerumani.

No comments:

Post a Comment