STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 22, 2013

Kemmy atamba 'Nguvu ya Imani' ni rasharasha tu

Kemmy katika pozi
MSANII wa zamani wa kundi la Kaole Sanaa, Juliet Samson 'Kemmy', amesema kazi yake mpya anayotarajia kuiingiza sokoni ya 'Nguvu ya Imani' ni mwanzo wa kurudi kwenye 'gemu' baada ya mashabiki wake kumkosa kwa muda mrefu.
Alisema amevunja ukimya kwa kupakua filamu hiyo aliyowashirikisha wasanii kadhaa wanaotamba nchini ili kuthibitisha kuwa bado wamo, tofauti na watu wanavyodhani kuwa enzi zake zimeisha.
"Hizi ni salamu na mvua za rasharasha tu, kuna makubwa yanakuja ndani ya 2013 baada ya 'Nguvu ya Imani'," alisema Kemmy.
Kemmy ambaye ni mtunzi, muandaaji na muongozaji kwa sasa, alisema zipo kazi nyingine zilizokaa tayari kuachiwa mara zitakapokamilika, lakini amefungua pazia na filamu hiyo ambayo hivi karibuni itakuwa mtaani.
Filamu hiyo inayohusu simulizi la wanawake wa jamii ya wafugaji na aina ya misukosuko wanayokumbana katika maisha yao ya kila siku ameiigiza yeye (Kemmy),  Simon Mwapangata maarufu kama 'Rado', Jackson Kabigili na wengine.

1 comment:

  1. Eeh Mudada huyu bado yupo, kapendezaje jamani? Tunaisubiri kwa hamu hiyo Nguvu ya Imani tuone makali yako mpendwa.
    Mama Sakina, Tabata

    ReplyDelete