STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 20, 2013

BIBI CHEKA SASA ANALIA, KISA...!

Bibi Cheka (kulia) akiwa na Fella

BAADA ya kutambulishwa vyema na nyimbo zake mbili za 'Ni Wewe' alioimba na Mheshimiwa Temba na 'Good Baba Fella' aliomshirikisha rapa Godzilla, msanii mwenye umri mkubwa, Cheka Hijja 'Bibi Cheka' amefyatua wimbo mpya uitwao 'Nalia'.
Akizungumza na MICHARAZO, meneja wa msanii huyo, Said Fella alisema wimbo huo pamoja na video yake imekamilika wiki iliyopita na unatarajiwa kuachiwa rasmi kwa mashabiki leo Jumatano.
Fella alisema Bibi Cheka anayetokea katika kituo chake cha Mkubwa na Wanawe, safari hii ametoa kazi hiyo akiimba yeye peke yake tofauti na 'ngoma' zake za awali ambazo zinaendelea kutamba.
Alisema wimbo huo ni wa tatu kwa msanii huyo anayeshikilia rekodi ya kuwa msanii mzee zaidi kuimba nyimbo za vijana.
Katika hatua nyingine, Fella alisema wimbo wao mpya wa 'Bendera' ulioimbwa na wasanii kadhaa wa Mkubwa na Wanawe, umeshasambazwa na kuanza kusikika hewani wakati wakijiandaa kutoa video yake.
"Tayari tumeshausambaza wimbo wa 'Bendera' na umeanza kusikika hewani. Sasa tunajiandaa kurekodi video yake mara baada ya kumalizika kwa Pasaka," alisema Fella

No comments:

Post a Comment