STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 20, 2013

KR Mullah ana wivu kwa masela



NYOTA wa muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la Wanaume Halisi, Rashidi Ziada maarufu kama KR Mullah, amesema anajiandaa kutoa nyimbo zake mbili binafsi ziitwazo 'Wivu' na 'Masela na Machizi'.
Akizungumza na MICHARAZO, KR alisema amemaliza kuzifanyia mazoezi nyimbo hizo na zitarekodiwa baada ya kiongozi wao wa kundi la Wanaume Halisi, Sir Juma Nature, atakapomaliza uzinduzi wa albamu yake binafsi.
KR Mullah ambaye pia ni mwanasoka, alisema ndani ya kundi lao wamewekeana utaratibu wa kila mwanakundi kutoa kazi binafsi na kwa sasa ni zamu ya Nature kisha itafuata yake.
"Natarajia kuvunja ukimya tangu nilipoachia wimbo wa 'Choo cha Kike' kwa kutoa nyimbo mbili za 'Wivu' na 'Masela na Machizi', ambazo zimekamilika mashairi yake isipokuwa nasubiri kuzipeleka studio baada ya Nature kutoka," alisema.
Mkali huyo, mmoja wa waasisi wa kundi la TMK Wanaume Halisi 'Mapanga Shaa' alisema imani yake ni kwamba nyimbo hizo zitarejesha heshima aliyopata kupitia kazi zake za awali ukiwamo wa 'Kamua kwa Uwezo'.
"Kwa wanaonifahamu nadhani wanajua namaanisha nini ninapowaambia wajiandae kupata burudani kutoka kwangu, ila kifupi ni kwamba 'Wivu' na 'Masela na Machizi' zitakuwa zaidi ya burudani," alisema.

No comments:

Post a Comment