STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 20, 2013

Simba yainyuka CDA, leo kuikabili Singida Utd


SIMBA ilipata ushindi wa bao 1-0 juzi katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya CDA ya Dodoma na leo inatarajia kushuka tena dimbani kwenye uwanja wa Namfua mkoani Singida kuikabili Singida United.
Bao pekee la Simba katika mechi yao dhidi ya CDA kwenye Uwanja wa Jamhuri lilifungwa katika kipindi cha kwanza na winga wao Kigi Makasi.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Said Pamba, ambaye yuko na timu katika safari yao itakayowafikisha hadi Bukoba mkoani Kagera, aliliambia gazeti hili jana kwamba  wameshatua Singida na wachezaji wote wako katika hali nzuri.
Pamba alisema kwamba bado kikosi hicho kiko chini ya uongozi wa mwenyekiti Ismail Aden Rage, na hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika kama ilivyotangazwa na baadhi ya wanachama waliokutana Jumapili na kudai wamewang'oa madarakani viongozi halali waliopo.
Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara wanatumia mechi hizo za kirafiki kuiandaa timu yao kabla ya kukutana na Kagera Sugar katika mechi ya ligi kuu itakayochezwa Machi 27 kwenye Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.
Baada ya mechi yao dhidi ya Kagera, Simba itaelekea Mwanza kuivaa Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, mechi itakayochezwa Machi 30.


CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment