STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 20, 2013

Kibwende cha Kazi chatoka


MCHEKESHAJI anayetamba na filamu kadhaa za komedi, Kazi Seleman 'Kazi' ameachia wimbo mpya wa muziki wa kizazi kipya uitwao 'Kibwende' alioimba na wasanii wenzake wa 'Vituko Show', Man Bizzo na Tausi.
Kazi, msanii mwenye umbile dogo alisema wimbo huo ameurekodi mjini Tanga na anatarajia kuanza kuusambaza ili urushwe hewani wakati akijiandaa kurudi tena studio kufyatua mwingine akimshirikisha nyota, Prince Dully Sykes.
Msanii huyo aliutaja wimbo huo anaojiandaa kuurekodi kuwa ni 'Mateso' utakaokuwa katika miondoko mchanganyiko ya Kwaito na Rhumba.
"Nimekamilisha wimbo wangu mpya uitwao 'Kibwende' nilioimba na 'swahiba' yangu Man Bizzo na Tausi, wakati pia najiandaa kurudi studio kurekodi kazi nyingine ambayo nimepanga kuimba na Dully Sykes," alisema Kazi

No comments:

Post a Comment