STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 20, 2013

Star Boy ajifua kumkabili Yusuf Jibaba



BONDIA Shabani Mhamila 'Star Boy' ameingia kambini kujiandaa 

kumkabili Yusuf Jibaba katika pambano la utangulizi wakati wa
mchezo wa kati ya Francis Cheka na Thomas Mashali.
Pambano hilo la raundi nne linatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa PTA Sabasaba, Dar es Salaam Mei Mosi mwaka huu, linatarajiwa kuwa la vuta nikuvute kutokana na kila mmoja kujigamba kujiandaa vema.
Kocha wa Star Boy, Habibu Kinyogoli 'Master' akisaidiwa na  Rajabu Mhamila 'Super D' wamesema kuwa bondia wao ameingia kambini juzi kujiandaa kumchakaza Jibaba ili
kuendelea kujiwekea sifa nzuri.
"Bondia wangu yuko katika maandalizi ya kutosha kuhakikisha anafanya vizuri katika pambano hilo la utangulizi kati ya Cheka na  Mashali" alisema Super D na kuongeza Star Boy alishawahi kuwa
bingwa wa masumbwi mwaka 1998.
Hata hivuo aliamua kusimama kwa muda kucheza ngumi na kwa sasa amerejea ulingoni ili atoe changamoto za mchezo huo.
Bondia huyo mwenye rekodi ya kucheza mapambano 23 akishinda 14 (5 KO) kupoteza 7 na kupata sare mbili.
Super D, kocha huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini, alisema kuwa katika mchezo huo kutakuwa na DVD za mafunzo ya mchezo huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi. 
DVD hizo zinahusisha mapambano ya Kalama Nyilawila dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na Francis Miyeyusho, Said Mundi na King Class Mawe.

No comments:

Post a Comment